William Ruto na Gideon Moi wakutana

0

Naibu wa Rais William Ruto  na seneta wa Baringo  Gedion Moi wamekutana katika mazishi ya  aliyekuwa mwanasiasa Hosea Kiplagat katika kaunti ya Baringo.

Ruto ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa vijana kujiunga na taasisi za kiufundi ili kupata mafunzo yatakayowawezesha kupata ajira.

Aidha Ruto amesema kuwa serikali bado itaendelea  kufanya maendeleo ya ujenzi wa barabara na kuhakikisha wakaazi  hao wamepata umeme.

Kiplagat aliaga dunia tarehe 6 mwezi huu akipokea matibabu katika hospitali ya Kareni .

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here