FIFA YAONDOA MARUFUKU DHIDI YA KENYA

0

Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA limeondoa marufuku iliyowekwa dhidi ya taifa la Kenya mwezi wa Februri mwaka huu.

FIFA Kupitia barua kwa katibu mkuu wa shirikisho la Soka humu nchini FKF Barry Otieno limesema litatuma ujumbe humu nchini kujadili hatua za kurejesha Kenya katika soka ya kimataifa..

Ktaibu mkuu wa  Shirikisho hilo Fatma Samoura aidha amesema  wataandaa  mkutano  na waziri wa Spoti Ababu Namwamba kuhusu maswala ya usimamizi wa soka humu nchini.

Kenya ilipigwa marufuku baada ya vuta nkuvute kati ya FKF ikiongozwa na Nick Mwendwa na waziri wa    Michezo  wa zamani Amina Mohammed.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here