KAMATI YA LEBA YAWAGIZA WAZIRI MBADI NA OPARANYA KUFIKA MBELE YAKE

0

Kamati ya Leba kwenye bunge la seneti imewaagiza Waziri wa fedha John Mbadi, Waziri wa vyama vya ushirika Wycliffe Oparanya na Meneja Mkurugenzi wa shirika la reli (KRC) Phillip Mainga kufika mbele yake kueleza sababu ya kucheleweshwa kwa malpo ya wafanyikazi waliostaafu wa shirika la reli la Kenya

Kamati hiyo inayoongozwa na Seneta wa Pokot Magharibi Julius Murgor imemwonya watatu hao kuwa iwapo hawatafika kwenye kikao hicho watatozwa faini ya shilingi elfu 500

Mbadi anatarajiwa kutoa maelezo kuhusu malipo ya shilingi bilioni 2.6 kwa madiwani wa zamani na pensheni ya kila mwezi kwa wastaafu elfu 11,900 wakiwemo waliokuwa wafanyikazi wa shirika la reli

Ikumbukwe awali Waziri Mbadi amekosa kuhudhuria vikao viwili mfululizo kikiwemo kile cha Julai 31 na Agosti 4 2025.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here