Rais Uhuru Kenyatta ameonekana kutofautiana na hatua ya idara ya upelelezi nchini DCI kufufua kesi zinazohusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007.

Badala yake rais amesema Wakenya tayari wamesahau yaliyopita na halitakuwa jambo la busara kurejea mahali taifa limetoka.

Mkurugenzi mkuu wa DCI George Kinoti anasema idara hiyo inachunguza madai ambapo baadhi ya watu wameanza kupokea vitisho kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022.